Thursday , 9 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Senegal yatangaza mapumziko baada ya kushinda Afcon
KimataifaMichezo

Senegal yatangaza mapumziko baada ya kushinda Afcon

Spread the love

 

RAIS wa Senegal, Macky Sall ametangaza leo Jumatatu tarehe 7 Februari, 2022 kuwa siku ya mapumziko kusherehekea ushindi wa timu ya taifa wa Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Rais Sall ambaye alikuwa nje ya nchi amefutilia mbali awamu ya mwisho ya safari yake katika Visiwa vya Comoro na kurejea nchini mwake kuwapokea nyota hao wa soka kurejea nchini leo.

Kwa mujibu wa Televisheni ya Taifa – RTS, Rais Sall pia kesho Jumanne ataiandalia dhifa maalumu Ikulu.

Senegal imeshinda fainali ya kwanza ya Afcon baada ya kushindwa mara mbili katika fainali za mwaka 2002 na 2019.

Waliishinda Misri 4-2 kwa mikwaju ya penalti na kupata ushindi wao baada ya fainali kumalizika bila bao kufuatia muda wa nyongeza.

Wakati huo huo, raia wameendelea kusherehekea usiku kucha kuamkia leo Jumatatu katika miji mbalimbali nchini Senegal kufuatia ushindia wa Kombe la Mataifa ya Afrika.

Kocha wa Senegal Aliou Cissé kipindi akiwa mchezaji alikosa penalti muhimu fainali za mwaka 2002 na kushindwa kubeba kombe hilo la Afcon.

Akiwa kama kocha, timu hiyo ilishindwa katika fainali ya mwaka 2019.

Senegal na Misri zitakutana tena katika mechi nyingine mwezi ujao kwenye mchujo wa kuwania kufuzu kwa Kombe la Dunia 2022 nchini Qatar.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Michezo

Piga pesa na mechi za UEFA

Spread the love  HATIMAYE leo hii ndio kitaeleweka nani aende Nusu Fainali...

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

error: Content is protected !!