Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mafao ya Ndugai balaa, kuvuna mamilioni
Habari za Siasa

Mafao ya Ndugai balaa, kuvuna mamilioni

Aliyekuwa Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai
Spread the love

 

ALIYEKUWA Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai ambaye alilazimika kujiuzulu wiki iliyopita, atavuna mamilioni ya shilingi kila mwezi, kama malipo yake ya kustaafu, ikiwamo asilimia 80 ya mshahara wa Spika atakayekuja kurithi nafasi yake hadi kifo. Anaripoti Gabriel Mushi…(endelea).

Taarifa kutoka bungeni Dodoma na serikalini zinasema, pamoja na kujiuzulu wadhifa wake, Ndugai atalipwa asilimia 50 ya mafao ya fedha alizopata akiwa Spika.

Kwa mujibu wa Sheria ya viongozi wastaafu wa kisiasa ya mwaka 1999, inayozungumzia mafao ya Spika, inaeleza kuwa kiongozi anayeacha nafasi ya Spika wa Bunge, atakuwa na haki ya kupata mafao yafuatayo, baada ya kuacha nafasi hiyo.

Kifungu cha 18 (a) kinasema, kiongozi aliyeshika nafasi ya madaraka ya Spika wa Bunge, baada ya kuacha wadhifa huo, atapewa kiinua mgongo asilimia 50 ya fedha zote, alizowahi kupokea kama mishahara wakati akiwa Spika.

Undani wa habari hii kujua mgawanyo wa mamilioni hayo, soma gazeti la Raia Mwema la leo Jumatatu, 10 Januari 2022.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!