Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mafao ya Ndugai balaa, kuvuna mamilioni
Habari za Siasa

Mafao ya Ndugai balaa, kuvuna mamilioni

Aliyekuwa Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai
Spread the love

 

ALIYEKUWA Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai ambaye alilazimika kujiuzulu wiki iliyopita, atavuna mamilioni ya shilingi kila mwezi, kama malipo yake ya kustaafu, ikiwamo asilimia 80 ya mshahara wa Spika atakayekuja kurithi nafasi yake hadi kifo. Anaripoti Gabriel Mushi…(endelea).

Taarifa kutoka bungeni Dodoma na serikalini zinasema, pamoja na kujiuzulu wadhifa wake, Ndugai atalipwa asilimia 50 ya mafao ya fedha alizopata akiwa Spika.

Kwa mujibu wa Sheria ya viongozi wastaafu wa kisiasa ya mwaka 1999, inayozungumzia mafao ya Spika, inaeleza kuwa kiongozi anayeacha nafasi ya Spika wa Bunge, atakuwa na haki ya kupata mafao yafuatayo, baada ya kuacha nafasi hiyo.

Kifungu cha 18 (a) kinasema, kiongozi aliyeshika nafasi ya madaraka ya Spika wa Bunge, baada ya kuacha wadhifa huo, atapewa kiinua mgongo asilimia 50 ya fedha zote, alizowahi kupokea kama mishahara wakati akiwa Spika.

Undani wa habari hii kujua mgawanyo wa mamilioni hayo, soma gazeti la Raia Mwema la leo Jumatatu, 10 Januari 2022.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!