Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Shughuli za Bunge zasimamishwa Tanzania
Habari za SiasaTangulizi

Shughuli za Bunge zasimamishwa Tanzania

Bunge la Tanzania
Spread the love

 

KATIBU wa Bunge la Tanzania, Nenelwa Mwihambi ametangaza kusitisha shughuli zote za Bunge ikiwemo kamati za Bunge zilizokuwa zikutane kuanzia tarehe 10 Januari 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kamati hizo, zilikuwa zinakutana kwa ajili ya maandalizi ya mkutano wa Bunge utakaoanza tarehe 1 Februari 2022.

Taarifa ya Nenelwa aliyoitoa leo asubuhi Ijumaa tarehe 7 Januari 2022, imesema amechukua uamuzi huo baada ya aliyekuwa spika, Job Ndugai kujiuzulu nafasi hiyo jana Alhamisi.

Spika wa Bunge, Job Ndugai

Amesema kwa mujibu wa Ibara ya 84(1) ya Katiba ya Tanzania yam waka 1997, Spika ndiye kiongozi wa Bunge na ndiye msimamizi wa shughuli zote za Bunge.

Aidha, Ibara ya 84(8) inaelekeza kwamba kiti cha spika kinapokuwa wazi hakuna shughuli yoyote itakayotekelezwa katika Bunge isipokuwa uchaguzi wa Spika.

Amewataka wabunge kuwasili Dodoma tarehe 31 Januari 2021.

Kwa maana hiyo, mara ya Bunge kukutana tarehe 1 Februari 2021, shughuli ya kwanza itakuwa kumchagua spika.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!