Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wadau waanza kutoa maoni maboresho sheria ya uhujumu uchumi Zanzibar
Habari za Siasa

Wadau waanza kutoa maoni maboresho sheria ya uhujumu uchumi Zanzibar

Spread the love

 

WADAU kutoka katika Asasi za Kiraia, wameanza kutoa maoni yao juu ya marekebisho ya Sheria ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Maoni hayo yametolewa leo Jumamosi, tarehe 18 Desemba 2021 katika mkutano wa wadau wa Asasi za Kiraia, uliuofanyika kwenye Hoteli ya Golden Tulip, visiwani Zanzibar.

Mkutano huo umeandaliwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, kupitia Tume ya Marekebisho ya Sheria visiwani humo, kwa kushirikiana na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC)-Zanzibar na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Zanzibar (ANGOZA).

Akizungumza katika mkutano huo, Katibu Tume ya Kurekebisha Sheria Zanzibar, Mussa Kombo Bakari, amesema mkutano huo utasaidia kupata maoni yatakayoboresha sheria hiyo.

“Mapambano dhidi ya rushwa hayawezi kufanikiwa kama players (wachezaji) muhimu kama ninyi, kwa maana ya asasi za kiraia hamtashiriki kikamilifu, kwa hiyo wao wenyewe kutumia utalaamu wao isingekuwa rahisi, pengine mafanikio tunayopata yawezekana hatujapata asilimia kubwa pengine baada ya mkutano huu tunaweza kushauriana tukafika mbali zaidi,” amesema Bakari.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!