Saturday , 4 May 2024
Home Gazeti Habari Rais Samia: Machinga tuendelee kuvumiliana
HabariTangulizi

Rais Samia: Machinga tuendelee kuvumiliana

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa rai kwa wafanya biashara wadogo wadogo ‘machinga’ kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kwa kuwa kazi ya kuwaondoa barabarani ni kwa nia njema ya maendeleo yao wenyewe hapo baadae. Anaripoti Matilda Buguye… (endelea)

Pia amesema uamuzi wa Serikali unalenga kuwajengea mazingira na sasa inaendelea kukusanya fedha kwa ajili ya kuwajengea maeneo mazuri na yakudumu kwa ajili ya biashara zao. 

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 4 Disemba, 2021 katika hafla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa miundombinu ya mabasi yaendayo haraka awamu ya pili, Mbagala rangi tatu jijini Dar es salaam.

Huku akiambatana na viongozi mbalimbali wa serikali katika hafla hiyo iliyopambwa na vikundi mbalimbali vya burudani ilivyoshuhudiwa na wananchi wa Mbagala walioweza kuhudhuria kwenye hafla hiyo.

Aidha, Rais Samia awakemea baadhi ya wananchi wasiokua na uzalendo ambao wanajihusisha na kuhujumu jitihada za utekelezaji wa mradi  huo wa ujenzi kwa kufanya vitendo vya wizi wa vifaa mbalimbali vinavyotumika.

Hivyo awaomba wananchi walio na uzalendo watakapogundua juu ya uhujumu wa aina yeyote juu ya ujenzi huo waseme na kutoa taarifa sehemu husika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

error: Content is protected !!