Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Wanafunzi wapya Chuo cha Mwalimu Nyerere wakaribishwa kwa ujumbe
ElimuHabari za Siasa

Wanafunzi wapya Chuo cha Mwalimu Nyerere wakaribishwa kwa ujumbe

Spread the love

 

MKUU wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam, Prof Shadrack Mwakalila amewataka wanafunzi wa chuo hicho kujiepusha na masuala ya kisiasa na wajielekeze katika mambo ya msingi yanayohusiana na taaluma ili kupata maarifa bora yatakayowasaidia katika maisha yao na taifa kwa ujumla. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Amesema hayo leo Jumatano, tarehe 24 Novemba 2021, wakati akiwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa chuo hicho na kusisitiza chuo hicho hakiruhusu itikadi za siasa.

Profesa Mwakalila amesema, ndiyo maana wakati wa udahili hakuna mwanafunzi aliyeulizwa chama anachotoka. Pia, amewaasa wafanyakazi wote wa chuo hicho kutoa huduma bora kwa wanafunzi ili waweze kusoma na kupata maarifa bora.

“Ili uweze kupata maarifa bora lazima mwanafunzi usome kwa juhudi na maarifa, uwe muadilifu na mzalendo hii itakusaidia wewe na Taifa, jiepusheni na makundi ya uchochezi na mzingatie zaidi masomo pamoja na kujiepusha na udanganyifu wowote kwenye mitihani,” amesema Prof. Mwakalila.

Aidha, Prof. Mwakalila amewataka watumishi wa chuo hicho kutoa huduma zilizo bora kwa wanafunzi wote ili kujenga Taifa lenye wataalamu wenye uwezo wa kuchangia maendeleo ya Taifa.

Mkuu huyo wa chuo ameahidi uongozi wa chuo utahakikisha unaboresha mazingira ya kujifunzia ili kila mwanafunzi aweze kupata maarifa bora katika mazingira bora.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!