Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko TCRA, TUZ wakutana Dar
Habari Mchanganyiko

TCRA, TUZ wakutana Dar

Spread the love

 

WAJUMBE wa Bodi, Menejimenti na Wafanyakazi wa Tume ya Utangazaji Zanzibar (TUZ) wametembelea Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Wajumbe ho wamepokelewa na viongozi mbalimbali wa TCRA, akiwemo Mkurugenzi Mkuu, Dk. Jabiri Bakari ambaye na kuwaeleza jinsi mamlaka hiyo inavyofanya kazi zake.
Katika ziara hiyo, TCRA na TUZ wameashiria nia ya kuhuisha baadhi ya vipengele vya mashirikiano baina ya taasisi hizo mbili kwa lengo la kuboresha huduma wanazosimamia.

Pia, wamepata ufafanuzi juu ya mfumo wa ugawaji na usimamizi wa masafa, utangazaji na utoaji wa leseni za mawasiliano

TUZ imeweka bayana dhamira yake ya kuboresha zaidi huduma zake mara baada ya ziara hiyo ya mafunzo ikiwemo utoaji huduma za mawasiliano pamoja na maandalizi ya kupokea mabadiliko ya TEHAMA katika kuboresha sekta ya mawasiliano Zanzibar.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!