Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko TCRA, TUZ wakutana Dar
Habari Mchanganyiko

TCRA, TUZ wakutana Dar

Spread the love

 

WAJUMBE wa Bodi, Menejimenti na Wafanyakazi wa Tume ya Utangazaji Zanzibar (TUZ) wametembelea Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Wajumbe ho wamepokelewa na viongozi mbalimbali wa TCRA, akiwemo Mkurugenzi Mkuu, Dk. Jabiri Bakari ambaye na kuwaeleza jinsi mamlaka hiyo inavyofanya kazi zake.
Katika ziara hiyo, TCRA na TUZ wameashiria nia ya kuhuisha baadhi ya vipengele vya mashirikiano baina ya taasisi hizo mbili kwa lengo la kuboresha huduma wanazosimamia.

Pia, wamepata ufafanuzi juu ya mfumo wa ugawaji na usimamizi wa masafa, utangazaji na utoaji wa leseni za mawasiliano

TUZ imeweka bayana dhamira yake ya kuboresha zaidi huduma zake mara baada ya ziara hiyo ya mafunzo ikiwemo utoaji huduma za mawasiliano pamoja na maandalizi ya kupokea mabadiliko ya TEHAMA katika kuboresha sekta ya mawasiliano Zanzibar.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

error: Content is protected !!