Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Samaki aibua hofu, akikung’ata huonani na mkeo miezi 6
Habari Mchanganyiko

Samaki aibua hofu, akikung’ata huonani na mkeo miezi 6

Spread the love

 

SAMAKI ni kitoweo pendwa kwa watu wengi duniani, hususani wakazi wa maeneo ya pwani na kando ya mito na maziwa. Lakini kwa wakazi wa Lamu nchini Kenya, samaki aina ya taa ni hatari pale anapokung’ata anasababisha usishiriki tendo la ndoa na mkeo kwa muda wa miezi sita. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea)

Hali hiyo imeibua hofu kwa wanaume wakazi wa Kaunti hiyo la Lamu kwa sababu ni tisho kubwa kwa maisha yao na ya kifamilia.

Samaki huyo aina ya taa ni mkubwa na mwenye umbo bapa na mkia mrefu ambao ncha yake ina maumbile kama ukucha unaoaminika kuwa na sumu kali.

Wakazi wa Lamu wanaamini anayedungwa na taa hastahili kushiriki mapenzi na mkewe kwa karibu miezi sita wakati akiuguza kidonda.

Mzee wa kisiwa cha Kizingitini, Khaldun Vae amewaeleza waandishi wa habari nchini humo kuwa imani hiyo imekita mizizi tangu enzi za mababu katika vijiji vyao.

“Baadhi ya ndoa zimekuwa zikiyumba punde waume wanapojeruhiwa na samaki huyo.

“Tangu enzi za mababu zetu, huwezi kudungwa na mwiba wa taa na kabla hujapona unakimbilia kulala na mkeo. Huko ni kujichimbia kaburi,” alisema Vae.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

error: Content is protected !!