Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Staa wa movi aua mwanamke kwa bunduki wakati wa kutengeneza filamu
KimataifaMichezo

Staa wa movi aua mwanamke kwa bunduki wakati wa kutengeneza filamu

Alec Baldwin
Spread the love

 

MWANAMKE  mmoja amefariki dunia huku mwanaume mmoja akijeruhiwa baada ya muigizaji Alec Baldwin kufyatua risasi kwa kutumia bunduki ya maigizo wakati wakiandaa filamu yao huko New Mexico nchini Marekani. Anaripoti Mwandishi wetu… (endelea).

Polisi katika jimbo hilo la Marekani wamesema Baldwin alitoa silaha hiyo wakati wa utengezaji wa filamu yake.

Mwanamke huyo alipelekwa hospitalini lakini alifariki kutokana na majeraha aliyopata.

Hata hivyo, mwanaume aliyejeruhiwa – ambaye ni mkurugenzi wa filamu, alikuwa akipokea huduma ya dharura.

Msemaji wa Baldwin aliliambia shirika la habari la AP kwamba kisa hicho kilihusisha utumiaji mbaya wa bunduki ya maigizo.

Mwanamke huyo ametajwa kama Halyna Hutchins (42), ambaye alikuwa akifanya kazi kama mkurugenzi wa upigaji picha. Mtu anayetibiwa ni Joel Souza (48), mkurugenzi wa filamu.

Polisi wamesema bado wanachunguza tukio hilo huko Bonanza Creek Ranch, eneo maarufu la utengenezaji wa sinema, na hakuna mashtaka yoyote yaliyofunguliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!