Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Staa wa movi aua mwanamke kwa bunduki wakati wa kutengeneza filamu
KimataifaMichezo

Staa wa movi aua mwanamke kwa bunduki wakati wa kutengeneza filamu

Alec Baldwin
Spread the love

 

MWANAMKE  mmoja amefariki dunia huku mwanaume mmoja akijeruhiwa baada ya muigizaji Alec Baldwin kufyatua risasi kwa kutumia bunduki ya maigizo wakati wakiandaa filamu yao huko New Mexico nchini Marekani. Anaripoti Mwandishi wetu… (endelea).

Polisi katika jimbo hilo la Marekani wamesema Baldwin alitoa silaha hiyo wakati wa utengezaji wa filamu yake.

Mwanamke huyo alipelekwa hospitalini lakini alifariki kutokana na majeraha aliyopata.

Hata hivyo, mwanaume aliyejeruhiwa – ambaye ni mkurugenzi wa filamu, alikuwa akipokea huduma ya dharura.

Msemaji wa Baldwin aliliambia shirika la habari la AP kwamba kisa hicho kilihusisha utumiaji mbaya wa bunduki ya maigizo.

Mwanamke huyo ametajwa kama Halyna Hutchins (42), ambaye alikuwa akifanya kazi kama mkurugenzi wa upigaji picha. Mtu anayetibiwa ni Joel Souza (48), mkurugenzi wa filamu.

Polisi wamesema bado wanachunguza tukio hilo huko Bonanza Creek Ranch, eneo maarufu la utengenezaji wa sinema, na hakuna mashtaka yoyote yaliyofunguliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!