Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo NBC yatumia bilioni 2.5 kudhamini ligi kuu
MichezoTangulizi

NBC yatumia bilioni 2.5 kudhamini ligi kuu

Spread the love

 

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) imeingia mkataba na Benki ya NBC wenye thamani ya Sh.2.5 bilioni bila Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kudhamini Ligi Kuu Tanzania Bara. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mkataba huo wa miaka mitatu umesainiwa leo Jumatano, tarehe 6 Oktoba 2021. Kila mwaka NBC itatoa Sh.2.5 bilioni.

TFF na NBC wameingia mkataba huo wakati tayari ligi kuu msimu wa 2021/22, yenye timu 16 imekwisha kuanza kwa michezo raundi ya kwanza na pili kupigwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi amesema, uamuzi wa kuamua kuwekeza katika mchezo wa mpira wa miguu kwa manufaa ya Taifa na “usitawi wa benki yetu” umetokana na ubora wa ligi hiyo.

“Tumefanya utafiti wa kutosha na kujidhihirisha, uimara wa uendeshwaji wa ligi na hivyo imekuwa rahisi zaidi kufanya uamuzi huu wa uwekezaji,” amesema Sabi

Sabi amesema, NBC imedhamilia kuwekeza kwa kipindi cha miaka mitatu lakini kwa mwaka 2021/22 imetoa Sh.2.5 bilioni “tukiamini, itaendeleza chachu ya mchezo wa soka Tanzania.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!