Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Jenerali Ulimwengu, Askofu Bagonza watoa somo madai ya katiba mpya
Habari za Siasa

Jenerali Ulimwengu, Askofu Bagonza watoa somo madai ya katiba mpya

Mwandishi wa habari mkongwe nchini, Jenerali Ulimwengu
Spread the love

 

ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Karagwe mkoani Kagera, Benson Bagonza na mwandishi wa habari mkongwe nchini, Jenerali Ulimwengu, wameonesha njia kuhusu suluhu ya madai ya katiba mpya. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza katika uzinduzi wa kitabu chake cha Rai ya Jenerali, leo Jumanne tarehe 21 Septemba 2021, jijini Mwanza, Ulimwengu ameshauri mabadiliko ya katiba yafanyike, ili kuziba mapungufu yake.

Ulimwengu amesema kuwa, mapungufu ya katiba yanayonekana kila siku kutokana na matumizi yake, hivyo kama yataonekana inatakiwa marekebisho yafanyike.

“Ni kweli na mimi huwa nasema katiba ni kitu ambacho kinaishi, mnaishi nacho siku zote na kila siku unapokitumia kitakuonesha kina mapungufu katika maeneo fulani fulani,” amesema Ulimwengu na kuongeza:

“Na hayo mapungufu yanaweza kuwa makubwa au madogo, kama madogo yanahitaji mabadiliko madogo madogo. Kama makubwa yanahitaji over roll na ifanyike.”

Askofu Benson Kagonza, KKKT Dayosisi ya Karagwe

Naye Askofu Bagonza, amesema ili katiba mpya ipatikane wanaohitaji mabadiliko hayo waibembeleze Serikali iliyopo madarakani.

“Hakuna uwezekano wa kupata katiba mpya nje ya CCM na hakuna uwezekano wa kuiondoa CCM bila katiba mpya, ni sawa na kuku na yai, kipi kina anza kuku au yai? ” amesema Askofu Bagonza na kuongeza:

“Nitalisema hili si kwa sababu nachukia jambo lolote, ninachotaka kusema inaonekana upinzani wa katiba uko ndani ya chama hicho. Ukitaka katiba mpya ni lazima ama uwabembeleze hawa au uwalazimishe.”

Madai ya katiba mpya yaliibuliwa hivi karibuni na baadhi ya vyama vya siasa vya upinzani, hasa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGO’s), wakidai katiba iliyopo ina mapungufu.

Hata hivyo, Rais Samia Suluhu Hassan aliwaomba watu wanaotaka katiba mpya wampe muda wa kuijenga nchi kiuchumi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!