Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makinda: Ni aibu kutohesabiwa
Habari za Siasa

Makinda: Ni aibu kutohesabiwa

Anna Makinda, Kamisaa wa Sensa Tanzania Bara
Spread the love

 

KAMISAA wa Sensa upande wa Tanzania Bara, Anne Makinda amewataka Watanzania wajione fahari kuhesabiwa kwa kuwa ni aibu kutohesabiwa katika sensa ya mwaka 2022. Anaripoti Glory Masamu TUDARCo … (endelea).

Makinda ambaye pia ni Spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, ametoa kauli hiyo leo tarehe 14 Septemba katika uzinduzi wa Kitabu cha Mkakati wa uelimishaji na uhamasishaji wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 jijini Dodoma.

Amesema sensa ya sasa itakuwa shirikishi na itaanzia ngazi ya vitongoji hivyo viongozi wa vitongoji vyote lazima watambue umuhimu wa zoezi hilo.

Ametoa wito kwamba siku ya kuhesabiwa itakapofika kila mtu akimbilie kuhesabiwa.

“Sensa itatufanya tujulikane tuko wangapi…kweli mwenyekiti wa kitongoji utashindwa kuwajua watu wako?

“Vitongoji wote tukihesabu watanzania wote watakuwa wamehesabiwa, mtanzania mwenzangu jitokeze uone fahari kuhesabiwa, ukiwa hukuhesabiwa usimwambie maana ni aibu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!