Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makinda: Ni aibu kutohesabiwa
Habari za Siasa

Makinda: Ni aibu kutohesabiwa

Anna Makinda, Kamisaa wa Sensa Tanzania Bara
Spread the love

 

KAMISAA wa Sensa upande wa Tanzania Bara, Anne Makinda amewataka Watanzania wajione fahari kuhesabiwa kwa kuwa ni aibu kutohesabiwa katika sensa ya mwaka 2022. Anaripoti Glory Masamu TUDARCo … (endelea).

Makinda ambaye pia ni Spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, ametoa kauli hiyo leo tarehe 14 Septemba katika uzinduzi wa Kitabu cha Mkakati wa uelimishaji na uhamasishaji wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 jijini Dodoma.

Amesema sensa ya sasa itakuwa shirikishi na itaanzia ngazi ya vitongoji hivyo viongozi wa vitongoji vyote lazima watambue umuhimu wa zoezi hilo.

Ametoa wito kwamba siku ya kuhesabiwa itakapofika kila mtu akimbilie kuhesabiwa.

“Sensa itatufanya tujulikane tuko wangapi…kweli mwenyekiti wa kitongoji utashindwa kuwajua watu wako?

“Vitongoji wote tukihesabu watanzania wote watakuwa wamehesabiwa, mtanzania mwenzangu jitokeze uone fahari kuhesabiwa, ukiwa hukuhesabiwa usimwambie maana ni aibu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!