Thursday , 9 May 2024
Home Kitengo Michezo Ndemla atua Mtibwa, Shikalo akitambulishwa KMC
MichezoTangulizi

Ndemla atua Mtibwa, Shikalo akitambulishwa KMC

Spread the love

 

MABINGWA wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara 2020/21, Simba ya jijini Dar es Salaam nchini Tanzania, imemtoa kwa mkopo wa mwaka mmoja kiungo wake mkabaji, Said Ndemla kwenda timu ya Mtibwa Sugar ya Morogoro. Anaripoti Damas Ndelema…(endelea).

Leo Jumamosi, tarehe 4 Septemba 2021, ukurasa wa Twitter wa Mtibwa Sugar umeweka picha za Ndemla akisaini mkabata wa kujiunga nao na kusema “tumefanikiwa kupata saini ya kiungo fundi mwenye hadhi ya juu kabisa nchini Said Ndemla kutoka Simba kwa mkopo wa mwaka mmoja.”

“Karibu sana Ndemla ufundi wako ukichanganywa na sukari yetu bora kabisa mambo yote yatakuwa,” imeeleza Mtibwa

Farouk Shikalo, Mlinda mlango mpya wa KMC

Wakati Ndemla, kiungo anayesifika kwa mashuti makali akitua kwa wakata miwa wa turiani, aliyekuwa kipa wa mabingwa wa kihistoria wa Tanzania, Yanga ya Dar es Salaam, Farouk Shikalo ametambulishwa na vijana wa Kinondoni, (KMC).

Farouk ambaye ni raia wa Kenya amejiunga na KMC baada ya mkataba wake wa miaka miwili ndani ya Yanga kumalizika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Michezo

Piga pesa na mechi za UEFA

Spread the love  HATIMAYE leo hii ndio kitaeleweka nani aende Nusu Fainali...

error: Content is protected !!