Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge CCM ataka zigo la kodi lihamishwe kwa wabunge
Habari za Siasa

Mbunge CCM ataka zigo la kodi lihamishwe kwa wabunge

Mbunge wa Ukonga (CCM), Jerry Slaa
Spread the love

 

Mbunge wa Ukonga (CCM), Jerry Slaa, ameshauri wabunge wakatwe kodi katika mishahara yao, ili wachangie maendeleo ya nchi, kama wananchi wanavyochangia kupitia tozo za miamala ya simu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Slaa ametoa ushauri huo jana tarehe 22 Julai 2021, akizungumza na wananchi wa Kata ya Mzinga, jijini Dar es Salaam.

“Ni wakati muafaka sisi wabunge tulipe kodi, ili tupate uwezo wa kusimama mbele ya watu kuwaambia walipe kodi. Na sisi tuanze kulipa kodi kwenye mishahara yetu,” alisema Slaa.

Slaa alisema, kama wabunge watakatwa kodi, italeta usawa kati wigo wa ulipaji kodi.

“Hakuna sababu ya kuwa na wengine hawalipi, ukishakuwa haulipi unakosa nguvu ya kuwaambia wengine walipe,” alisema Slaa.

Tozo hizo zinazotozwa katika miamala ya simu, zilianza kutumika kuanzia tarehe 15 Julai mwaka huu.

Ambapo Serikali inatoza kuanzia Sh. 10 hadi 10,000, katika muamala wa kutuma au kutoa pesa, kulingana na thamani ya muamala wa fedha husika.

1 Comment

  • Ni nchi gani wabunge hawalipi kodi?
    Hakika ni za Afrika, Asia na Amerika ya Kusini…ndiyo maana kuna umaskini wa serikali.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari za Siasa

Wizara ya Kilimo yapanga kutumia Sh. 1.2 trilioni 2024/25

Spread the loveWIZARA ya Kilimo, imepanga kutumia bajeti ya Sh. 1.2 trilioni...

error: Content is protected !!