Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Bosi Nida akalia kuti kavu, Waziri Simbachawene asema…
Habari Mchanganyiko

Bosi Nida akalia kuti kavu, Waziri Simbachawene asema…

Spread the love

 

WAZIRI wa Mambo ya Ndani nchini Tanzania, George Simbachawene, amemtaka Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dk. Anold Kihaule, akae kando kama kazi ya kuongoza mamlaka hiyo imemshinda. Anaripoti Mwandishi Wetu, Iringa … (endelea).

Simbachawene ametoa agizo hilo jana Jumatatu, tarehe 19 Julai 2021, katika ziara yake ya kikazi mkoani Iringa.

Simbachawene ametoa malekezo hayo baada ya kubaini changamoto katika utendaji wa NIDA, zilizopelekea mamlaka hiyo kushindwa kuzalisha vitambulisho vya Taifa vya kutosha.

“Tangu nimeingia kwenye uwaziri, kelele zote nilizopiga kuhusu vitambulisho zimezalisha milioni mbili. Siwezi kukubali ninachomwambia mkurugenzi kama kazi imemshinda awaachie watu wengine.”

“Ni mteule wa Rais lakini kama kazi imemshinda atafute kazi nyingine,” alisema Simbachawene.

Kwa mujibu wa Simbachawene, NIDA imetengeneza vitambulisho milioni mbili, idadi ndogo ikilinganishwa na mahitaji ya Watanzania wasiopungua milioni 50.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!