Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bosi Nida akalia kuti kavu, Waziri Simbachawene asema…
Habari Mchanganyiko

Bosi Nida akalia kuti kavu, Waziri Simbachawene asema…

Spread the love

 

WAZIRI wa Mambo ya Ndani nchini Tanzania, George Simbachawene, amemtaka Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dk. Anold Kihaule, akae kando kama kazi ya kuongoza mamlaka hiyo imemshinda. Anaripoti Mwandishi Wetu, Iringa … (endelea).

Simbachawene ametoa agizo hilo jana Jumatatu, tarehe 19 Julai 2021, katika ziara yake ya kikazi mkoani Iringa.

Simbachawene ametoa malekezo hayo baada ya kubaini changamoto katika utendaji wa NIDA, zilizopelekea mamlaka hiyo kushindwa kuzalisha vitambulisho vya Taifa vya kutosha.

“Tangu nimeingia kwenye uwaziri, kelele zote nilizopiga kuhusu vitambulisho zimezalisha milioni mbili. Siwezi kukubali ninachomwambia mkurugenzi kama kazi imemshinda awaachie watu wengine.”

“Ni mteule wa Rais lakini kama kazi imemshinda atafute kazi nyingine,” alisema Simbachawene.

Kwa mujibu wa Simbachawene, NIDA imetengeneza vitambulisho milioni mbili, idadi ndogo ikilinganishwa na mahitaji ya Watanzania wasiopungua milioni 50.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!