Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Vijana 200 wagawiwa fedha za kuoa
Kimataifa

Vijana 200 wagawiwa fedha za kuoa

Muhammad Bin Salman, Mwanamfalme wa Saudia
Spread the love

 

MUHAMMAD Bin Salman, Mwanamfalme wa Saudia, ameidhinisha kutolewa fedha milioni 3.74 za riyali, sawa na dola milioni 1 za kimarekani, ili zigawiwe kwa vijana 200 kama ruzuku ya kuoa. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Mtandao huo, umeripoti kwamba, Gazeti la Serikali la Saudi Arabia, limesema fedha hizo zitagawanywa kwa vijana wa kiume na wa kike kote nchini humo.

Limesema agizo la Mwanamfalme huyo ni katika juhudi za kuwasaidia yatima wenye ulemavu na watu wenye ulemavu ambao wamekuwa na shida ya kuoa.

Katika awamu ya kwanza ya mpango huo, riyali milioni 250 za msaada zilisambazwa, kwa watu zaidi ya 26,000 kutoka maeneo tofauti ya nchi hiyo.

Licha ya kupewa fedha, vijana watafundishwa jinsi ya kutumia fedha.

Mpango wa Mwanamfalme Muhammed Bin Salman ulianzishwa kwa lengo la kuimarisha uchumi na jamii ya watu wa nchi hiyo kuboresha maisha ya watu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!