Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwanamke anayetuhumiwa kumchomea ndani kwa petroli mpenzi wake akamatwa
Habari MchanganyikoTangulizi

Mwanamke anayetuhumiwa kumchomea ndani kwa petroli mpenzi wake akamatwa

Spread the love

 

POLISI Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia Grace Janes Mushi (25), kwa tuhuma za kumchoma moto ndani ya nyumba aliyekua mpenzi wake, Khamis Abdallah (25). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, Jumanne Muliro amesema, tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia jana Ijumaa tarehe 16 Julai 2021, majira ya saa 8:30 usiku, maeneo ya Mbezi Makabe kwa Mzungu Wilaya ya Ubungo.

Amesema, mtuhumiwa Grace majira hayo ya saa nane usiku aliamka na kumfungia mlango kwa nje Khamis Abdallah kisha kumwagia mafuta ya petroli nyumba hiyo, kitendo kilichosababusha Khamisi kuungua na  kufariki dunia akiwa ndani.

Kamanda Muliro amesema, uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa chanzo cha tukio hilo ni mgogoro wa kimapenzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

error: Content is protected !!