Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Ali Kiba akwaa ubalozi wa kinywaji
Michezo

Ali Kiba akwaa ubalozi wa kinywaji

Spread the love

 

MSANII wa muziki nchini Tanzania, Ali Kiba amesaini mkataba wa kinywaji cha “Power Horse” kuwa balozi wa kinywaji hicho. Anaripoti Matlida Peter, Dar es Salaam … (endelea).

Mkataba huo, umesainiwa leo Ijumaa, tarehe 16 Julai 2021, jijini Dar es Salaam, ikuhusika pande mbili za Ali Kiba na kampuni ya kinywaji hicho.

Mara baada ya kusaini mkataba huo, Ali Kiba amesema, atatumia nafasi hiyo kukitangaza kinywaji hicho nchi nzima.

https://www.youtube.com/watch?v=EOPcJvI6UZE

Msanii huyo, amewateua Mwijaku, Soudybrown, pamoja Danzak trainer kuwa wahamasishaji wa kinywaji hicho.

Awali, kampuni ya Power Horse imesema, imeamua kumchagua Ali Kiba kuwa balozi wao kutokana na umaarufu wake na ushawishi wake kwenye jamii.

Power Horse wamesema, Ali Kiba atatumia nafasi yake ya usanii kukitangaza vyema kinywaji hicho kisichokuwa na kilevi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!