Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia agonga siku 100 Ikulu
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia agonga siku 100 Ikulu

Samia Suluhu Hassan, akiapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Spread the love

 

LEO Jumapili, tarehe 27 Machi 2021, Samia Suluhu Hassan, ametimiza siku 100 tangu alipoapishwa kuwa Rais wa Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Aliapishwa tarehe 19 Machi 2021, Ikulu ya Dar es Salaam na Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma.

Ni baada ya kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli, kilichotokea saa 12 jioni ya tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam.

Mwili wa Hayati Magufuli, ulizikwa nyumbani kwao, Chato mkoani Geita.

Hayati John Magufuli

Samia, aliyekuwa makamu wa Rais, aliapishwa kuwa Rais kwa mujibu wa Katiba kisha yeye mwenyewe akamteua Dk. Philip Mpango, aliyekuwa waziri wa fedha na mipango kuwa makamu wa Rais.

Kesho Jumatatu, katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere, Dar es Salaam atazungumza na wahariri wa vyombo vya habari kuhusu siku 100 akiwa madarakani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!