
Samia Suluhu Hassan, akiapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
LEO Jumapili, tarehe 27 Machi 2021, Samia Suluhu Hassan, ametimiza siku 100 tangu alipoapishwa kuwa Rais wa Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Aliapishwa tarehe 19 Machi 2021, Ikulu ya Dar es Salaam na Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma.
Ni baada ya kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli, kilichotokea saa 12 jioni ya tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam.
Mwili wa Hayati Magufuli, ulizikwa nyumbani kwao, Chato mkoani Geita.

Samia, aliyekuwa makamu wa Rais, aliapishwa kuwa Rais kwa mujibu wa Katiba kisha yeye mwenyewe akamteua Dk. Philip Mpango, aliyekuwa waziri wa fedha na mipango kuwa makamu wa Rais.
Kesho Jumatatu, katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere, Dar es Salaam atazungumza na wahariri wa vyombo vya habari kuhusu siku 100 akiwa madarakani.
More Stories
#LIVE: Tuzo za EJAT2021, Majaliwa atoa ujumbe kwa MCT
Ni Profesa Hoseah tena TLS
Askofu Gwajima: Viongozi wa Serikali wanamchonganisha Rais