Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia agonga siku 100 Ikulu
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia agonga siku 100 Ikulu

Samia Suluhu Hassan, akiapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Spread the love

 

LEO Jumapili, tarehe 27 Machi 2021, Samia Suluhu Hassan, ametimiza siku 100 tangu alipoapishwa kuwa Rais wa Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Aliapishwa tarehe 19 Machi 2021, Ikulu ya Dar es Salaam na Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma.

Ni baada ya kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli, kilichotokea saa 12 jioni ya tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam.

Mwili wa Hayati Magufuli, ulizikwa nyumbani kwao, Chato mkoani Geita.

Hayati John Magufuli

Samia, aliyekuwa makamu wa Rais, aliapishwa kuwa Rais kwa mujibu wa Katiba kisha yeye mwenyewe akamteua Dk. Philip Mpango, aliyekuwa waziri wa fedha na mipango kuwa makamu wa Rais.

Kesho Jumatatu, katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere, Dar es Salaam atazungumza na wahariri wa vyombo vya habari kuhusu siku 100 akiwa madarakani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!