Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mzindakaya kuzikwa Alhamisi Rukwa
Habari Mchanganyiko

Mzindakaya kuzikwa Alhamisi Rukwa

Hayati Dk. Chrisant Mzindakaya
Spread the love

 

MWILI wa mwanasiasa mkongwe nchini Tanzania, Hayati Dk. Chrisant Mzindakaya (79), unatarajiwa kuzikwa Alhamisi tarehe 10 Juni 2021, nyumbani kwake Sumbawanga mkoani Rukwa. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumanne, tarehe 8 Juni 2021 na Msemaji wa Familia wa Mzindakaya, Kapteni Mstaafu, Zeno Nkoswe, akitangaza ratiba ya mazishi hayo, mkoani Rukwa.

Mzindakaya alifariki dunia Jumatatu, tarehe 7 Juni 2021, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, alikokuwa anapatiwa matibabu kwa zaidi ya mwezi mmoja.

Nkoswe amesema, kesho tarehe 9 Juni 2021, mwili wa Mzindakaya utasafirishwa kutoka Dar es Salaam, kuelekea mkoani Songwe kwa ndege, kisha utasafirishwa kwa gari kuelekea mkoani Rukwa, kwa ajili ya taratibu za mazishi.

“Maiti inategemewa kuja kesho kwa ndege, kutoka Dar es Saalam mpaka Songwe na kutoka Songwe maiti italetwa kwa barabara kuja Sumbawanga. Tunategemea kesho jioni maiti ya marehemu Mzindakaya inaweza ikawa imeingia hapa Sumbawanga,” amesema Nkoswe.

Msemaji huyo wa familia ya Mzindakaya, amesema baada ya mwili huo kuingia nyumbani kwake, Alhamisi itafanyika ibada ya mazishi.

“Baada ya mwili kuingia nyumbani kwake, pengine kesho kutwa tutafanya ibada na tutafanya mazishi nyumbani kwake hapa tulipo,” amesema Nkoswe.

Mzindakaya alikuwa mbunge kwa zaidi ya miaka 40, katika nyakati tofauti, kupitia majimbo ya mkoani Rukwa.(Ufipa Kusini, Sumbawanga Mjini, Nkasi na Kalambo).

Mwanasiasa huyo alizaliwa tarehe 31 Desemba 1940, mkoani Rukwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!