Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Changamoto za afya: Mbunge CCM awapigania wahitimu vyuo vikuu
Habari Mchanganyiko

Changamoto za afya: Mbunge CCM awapigania wahitimu vyuo vikuu

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mwanaidi Khamis
Spread the love

 

MBUNGE wa Viti Maalum (CCM), Latifa Juakali ameishauri Serikali ianzishe huduma ya bima ya afya, kwa wanafunzi wa elimu ya juu na wahitimu wanaosubiri kupata ajira, ili waondokane na changamoto za kumudu gharama za huduma ya afya. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Juakali ametoa ombi hilo leo Ijumaa tarehe 21 Mei 2021, bungeni jijini Dodoma, katika kipindi cha maswali na majibu.

“Je, Serikali ina mpango gani mahususi wa kuwapatia Bima ya Afya, wanafunzi wa
Elimu ya Juu na wanaosubiri kupata ajira?” amesema Juakali.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mwanaidi Khamis, amesema Serikali iko mbioni kuwasilisha bungeni muswada wa kutunga Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote, ili wanafunzi hao wanufaike na bima hizo.

“Kwa kutambua umuhimu wa kila mwananchi kuwa na Bima ya Afya, Serikali inakamilisha Rasimu ya Muswada wa kutunga Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote. Ambao utawasilishwa Bungeni mwezi Juni 2021,” amesema Mwanaidi.

Aidha, Mwanaidi amesema Serikali inatekeleza mpango wa Bima ya Afya kwa wanafunzi wa Elimu ya Juu, ambao hujiunga kwa kuchangia na kunufaika na huduma za bima ya afya kwa mwaka mzima.

Chuo Kikuu cha Dodoma

“Serikali imeendelea kuboresha huduma za bima ya afya, kwa kuongeza kitita cha huduma na upatikanaji wa huduma kwa wanachama kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, kwa kutekeleza mikakati mbalimbali yenye lengo la kuwawezesha wananchi wengi kujiunga na hivyo kuwa na uhakika wa kumudu gharama za matibabu,” amesema Mwanaidi.

Kuhusu wahitimu wanaosubiri kupata ajira, Mwanaidi amesema Serikali imeandaa utaratibu wa vifurushi vinavyowawezesha kupata bima hiyo.

“Kwa wale wanaosubiri kupata ajira, Mfuko umeandaa utaratibu wa Vifurushi ambavyo vimezingatia uhitaji wa aina ya huduma, umri na ukubwa wa familia. Kwa kumpatia mwananchi wigo wa kuchagua aina ya kifurushi kwa kulingana na mahitaji yake,” amesema Mwanaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!