Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Changamoto za afya: Mbunge CCM awapigania wahitimu vyuo vikuu
Habari Mchanganyiko

Changamoto za afya: Mbunge CCM awapigania wahitimu vyuo vikuu

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mwanaidi Khamis
Spread the love

 

MBUNGE wa Viti Maalum (CCM), Latifa Juakali ameishauri Serikali ianzishe huduma ya bima ya afya, kwa wanafunzi wa elimu ya juu na wahitimu wanaosubiri kupata ajira, ili waondokane na changamoto za kumudu gharama za huduma ya afya. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Juakali ametoa ombi hilo leo Ijumaa tarehe 21 Mei 2021, bungeni jijini Dodoma, katika kipindi cha maswali na majibu.

“Je, Serikali ina mpango gani mahususi wa kuwapatia Bima ya Afya, wanafunzi wa
Elimu ya Juu na wanaosubiri kupata ajira?” amesema Juakali.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mwanaidi Khamis, amesema Serikali iko mbioni kuwasilisha bungeni muswada wa kutunga Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote, ili wanafunzi hao wanufaike na bima hizo.

“Kwa kutambua umuhimu wa kila mwananchi kuwa na Bima ya Afya, Serikali inakamilisha Rasimu ya Muswada wa kutunga Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote. Ambao utawasilishwa Bungeni mwezi Juni 2021,” amesema Mwanaidi.

Aidha, Mwanaidi amesema Serikali inatekeleza mpango wa Bima ya Afya kwa wanafunzi wa Elimu ya Juu, ambao hujiunga kwa kuchangia na kunufaika na huduma za bima ya afya kwa mwaka mzima.

Chuo Kikuu cha Dodoma

“Serikali imeendelea kuboresha huduma za bima ya afya, kwa kuongeza kitita cha huduma na upatikanaji wa huduma kwa wanachama kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, kwa kutekeleza mikakati mbalimbali yenye lengo la kuwawezesha wananchi wengi kujiunga na hivyo kuwa na uhakika wa kumudu gharama za matibabu,” amesema Mwanaidi.

Kuhusu wahitimu wanaosubiri kupata ajira, Mwanaidi amesema Serikali imeandaa utaratibu wa vifurushi vinavyowawezesha kupata bima hiyo.

“Kwa wale wanaosubiri kupata ajira, Mfuko umeandaa utaratibu wa Vifurushi ambavyo vimezingatia uhitaji wa aina ya huduma, umri na ukubwa wa familia. Kwa kumpatia mwananchi wigo wa kuchagua aina ya kifurushi kwa kulingana na mahitaji yake,” amesema Mwanaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!