Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mlima Nkongore kumaliza mgogoro wa wananchi, Magereza
Habari Mchanganyiko

Mlima Nkongore kumaliza mgogoro wa wananchi, Magereza

David Silinde, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

 

SERIKALI iko katika hatua za mwisho kulifanya eneo la Mlima Nkongore mkoani Mara, kuwa hifadhi ya Taifa. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo Ijumaa tarehe 21 Mei 2021, bungeni jijini Dodoma, na Naibu Waziri Ofisi ya Rais-Tamisemi, David Silinde, akimjibu Mbunge wa Tarime Mjini (CCM), Mwita Michael, aliyehoji taratibu zilizotumika kuchukua ardhi hiyo kutoka kwa wananchi, na kulikabidhi kwa Jeshi la Magereza.

“Halmashauri ya Mji Tarime kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira, inakamilisha taratibu za kulifanya eneo la Mlima Nkongore kuwa hifadhi,” amesema Silinde.

Silinde amesema wananchi walinyang’anywa eneo hilo, baada ya kubainika wanafanya shughuli za kiuchumi zinazohatarisha mazingira ya Mlima Nkongore.

“Wananchi wanaozunguka eneo hilo walikuwa wakiutumia mlima huo kwa shughuli za kiuchumi ikiwemo ukataji kuni, uchomaji mkaa na kilimo, shughuli ambazo zilikuwa zinahatarisha mazingira yake,” amesema Silinde.

Pia, Silinde amesema eneo la mlima huo lilikuwa halijamilikishwa kwa wananchi kisheria na wala halikuwa na mipango miji.

“Mlima Nkongore una eneo lenye ukubwa wa ekari 266.65, eneo hilo halina mchoro wa mipango miji na halijamilikishwa,” amesema Silinde.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!