Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Mlima Nkongore kumaliza mgogoro wa wananchi, Magereza
Habari Mchanganyiko

Mlima Nkongore kumaliza mgogoro wa wananchi, Magereza

David Silinde, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

 

SERIKALI iko katika hatua za mwisho kulifanya eneo la Mlima Nkongore mkoani Mara, kuwa hifadhi ya Taifa. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo Ijumaa tarehe 21 Mei 2021, bungeni jijini Dodoma, na Naibu Waziri Ofisi ya Rais-Tamisemi, David Silinde, akimjibu Mbunge wa Tarime Mjini (CCM), Mwita Michael, aliyehoji taratibu zilizotumika kuchukua ardhi hiyo kutoka kwa wananchi, na kulikabidhi kwa Jeshi la Magereza.

“Halmashauri ya Mji Tarime kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira, inakamilisha taratibu za kulifanya eneo la Mlima Nkongore kuwa hifadhi,” amesema Silinde.

Silinde amesema wananchi walinyang’anywa eneo hilo, baada ya kubainika wanafanya shughuli za kiuchumi zinazohatarisha mazingira ya Mlima Nkongore.

“Wananchi wanaozunguka eneo hilo walikuwa wakiutumia mlima huo kwa shughuli za kiuchumi ikiwemo ukataji kuni, uchomaji mkaa na kilimo, shughuli ambazo zilikuwa zinahatarisha mazingira yake,” amesema Silinde.

Pia, Silinde amesema eneo la mlima huo lilikuwa halijamilikishwa kwa wananchi kisheria na wala halikuwa na mipango miji.

“Mlima Nkongore una eneo lenye ukubwa wa ekari 266.65, eneo hilo halina mchoro wa mipango miji na halijamilikishwa,” amesema Silinde.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Somo la dini: Waislamu waishukia Serikali, wizara yatoa kauli

Spread the loveJUMUIYA na Taasisi za Kiislamu Tanzania, imetupia lawama Serikali ikidai...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!