Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Viongozi wa dini wapewa ujumbe
Habari Mchanganyiko

Viongozi wa dini wapewa ujumbe

Spread the love

 

WATUMISHI wa Mungu, wameitwa duniani siyo kubomoa bali wanatakiwa kujenga ili watu waweze kumcha Mungu na kuachana na maovu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchungaji wa Kanisa la Maisha ya Ushindi lililopo eneo la Kigogo Freshi, Nelius Celemence amesema hayo hivi karibuni, alipokuwa kwenye ibada.

Amesema, mtumishi wa Mungu unapoanza kutoa maneno mabaya yanasababisha waumini kujigawa matokeo yake anabomoa badala ya kujenga.

Celemence alisema, kanisa la leo linahitaji maadili mema hasa kwa vijana, kina baba na mama ambao wanatakiwa kulifuata neno la Mungu litakalowasaidia kuondokana na matendo maovu ambayo hayampendezi Mungu.

“Kanisa la sasa linahitaji maneno mazuri na ya baraka na siyo maneno mabaya ya kuwasema watu na kuwakashifu na kuliponda neno la Mungu,”alisema Celemence.

Pia, aliwataka waumini kutafakari sheria za Mungu ambapo alitolea mfano kitabu cha Zabuni 1:1 hadi wa 6, Daudi anazungumzia kuhusu kukaa mbele ya mwenye mizaha.

Alisema mizaha inaondoa uwepo wa Mungu mfano mtumishi anapokaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!