Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Bosi zamani TRA ateuliwa Udart
Habari Mchanganyiko

Bosi zamani TRA ateuliwa Udart

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemteua Dk. Edwin Mhede kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (UDART). Anaripoti Hamis Mguta…(endelea).

Uteuzi wa Dk. Mhede, umetangazwa leo Jumamosi, tarehe 15 Mei 2021 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa ambaye amesema, anachukua nafasi ya John Nguya ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Kutenguliwa kwa uteuzi wa Nguya, umefanyika ikiwa ni takribani wiki mbili zimepita, tangu Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, kufanya ziara ya kutembelea mradi wa mabasi yaendayo haraka mkoani Dar es Salaam.

John Nguya

Katika ziara hiyo, Majaliwa alisema, Nguya ameshindwa kutimiza majukumu yake ipasavyo na kuufanya wakala huo, kutoa huduma chini na malengo na kuahidi kufikisha suala lake kwa mamlaka ya uteuzi kwa hatua zaidi.

Dk. Mhede, aliyekuwa Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ameteuliwa ikiwa zimepita siku 41 tangu alipomwondolewa TRA na nafasi yake kuteuliwa Alphayo Kidata.

Rais Samia, alimteua Kidata kuwa Kamishna wa TRA, tarehe 4 Aprili 2021.

Dk. Mhede, aliongoza TRA kuanzia 8 Januari 2019, akichukua nafasi ya Charles Kichere ambaye aliteuliwa kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Njombe. Kwa sasa Kichere ni Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Kabla ya uteuzi huo, Dk. Mhede alikuwa naibu katibu mkuu wizara ya viwanda na biashara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!