Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia awang’oa mabosi Takukuru, Bunge
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia awang’oa mabosi Takukuru, Bunge

Nenelwa Mwihambi, Katibu wa Bunge la Tanzania. 
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko ya Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Bunge la Tanzania. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Mabadiliko hayo, yametangazwa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, leo Jumamosi, tarehe 15 Mei 2021.

Katika mabadiliko hayo, Rais Samia amemtea Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Salum Rashid Hamduni kuwa Mkurugenzi Mkuu wa (Takukuru).

Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Salum Rashid Hamduni

Hamduni, anachukua nafasi ya Brigegia Jenerali John Mbungo ambaye atapangiwa majukumu mengine.

Pia, Hamduni amempandisha kuwa Kamishna wa Polisi (CP).

Brigedia Jenerali, John Mbungo

Katika mabadiliko mengine ambayo ameyafanya Rais Samia ni kumteua Nenelwa Mwihambi kuwa Katibu wa Bunge la Tanzania.

Nenelwa Mwihambi, Katibu wa Bunge la Tanzania.

Mwihambi alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Shughuli za Bunge-Ofisi ya Bunge, anachukua nafasi ya Stephen Kagaigai ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Kagaigai amekuwa kwenye nafasi hiyo tangu tarehe 7 Oktoba 2017, alipoteuliwa na aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati John Pombe Magufuli, kushika wadhifa huo, akichukua nafasi iliyokuwa imeachwa wazi na Dk. Thomas Kashillila, ambaye wakati huo, ilielezwa atapangiwa kazi nyingine.

Steven Kigaigai, aliyekuwa Katibu wa Bunge

Kabla ya kuteuliwa kuwa Katibu wa Bunge, Kagaigai alikuwa Kaimu Karani wa Baraza la Mawaziri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!