Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Warithi viongozi waliotimuliwa BAWACHA kupatikana Mei 18
Habari za Siasa

Warithi viongozi waliotimuliwa BAWACHA kupatikana Mei 18

Benson Kigaila, Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)
Spread the love

 

KAMATI Tendaji ya Baraza la Wanawake la Chadema (BAWACHA), tarehe 18 Mei 2021, itafanya uchaguzi kujaza nafasi za viongozi wa baraza hilo, waliofukuzwa uanachama Novemba 2020, kwa tuhuma za usaliti. Anripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa ya uchaguzi huo imetolewa leo Jumamosi tarehe 15 Mei 2021, na Naibu Katibu Mkuu Chadema Bara, Benson Kigaila.

“Kamati tendaji ya Baraza la Wanawake wa Chadema (BAWACHA) itakutana Jijini Mwanza tarehe 18 Mei 2021, kwaajili ya kufanya uchaguzi wa viongozi hao kwa mujibu wa muongozo wa baraza hilo kifungu cha 7.8.5 (a)(b)(c)(d),”imesema taarifa ya Kigaila.

Nafasi za Viongozi wa BAWACHA zitakazojazwa na Kamati yake Tendaji  ni, Ukatibu Mkuu, iliyokuwa inaongozwa na Grace Tendega, kabla hajafukuzwa Chadema.

Nafasi ya Unaibu Katibu Mkuu Bara, iliyokuwa chini ya Jesca Kishoa pamoja na Katibu Mwenezi, iliyokuwa imeshikwa na Agnesta Lambart.

Taarifa ya Kigaila imewataja wanachama wa Chadema walioteuliwa na Kamati Kuu ya chama hicho, kugombea nafasi hizo.

“Kamati kuu ya chama iliyokutana kidigitali tarehe 12 Mei 2021,  kwa mujibu wa kanuni za chama kifungu cha 7.2.6 pamoja na mambo mengine,  ilifanya usaili,  kujadili na kuteua wagombea wa nafasi mbali mbali zinazotarajiwa kufanyiwa uchaguzi katika BAWACHA,” imesema taarifa ya Bawacha.

Nafasi ya Ukatibu Mkuu BAWACHA, walioteuliwa kugimbea ni Asia Daud Msangi, Catherine Nyakao Ruge na Esther Cyprian Daffi.

Wakati Brenda Rupia Jonas, Emma Theobald Boki na Nuru Elias Ndosi, wakiteuliwa kugombea Unaibu Katibu Mkuu wa baraza hilo Bara, huku nafasi ya Unaibu Katibu Mkuu BAWACHA akiteuliwa Bahati Chum Haji, kugombea.

Halima Mdee

Kwa upande wa Katibu Mwenezi Bawacha, walioteuliwa kugombea ni,  Aisha Machano Ame, Husna Amri said na Sigrada Wilhem Mligo.

Nje ya Tendega na wenzake, viongozi wengine wa BAWACHA waliofukuzwa ni Halima Mdee, aliyekuwa Mwenyekiti wa baraza hilo Taifa na Hawa Mwaifunga (Makanu Mwenyekiti BAWACHA Zanzibar).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!