Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia aanza kuteua wapinzani
Habari za Siasa

Rais Samia aanza kuteua wapinzani

Qeen Cuthbert Sendiga- aliyekuwa mgombea urais 2020 kupitia ADC
Spread the love

 

SAMIA Suluhu Hassan, Rais  wa Tanzania, ameanza kutimiza ahadi yake ya kuteua wapinzani serikalini, baada ya kumteua Queen Cuthbert Sendiga, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar Es Salaam…(endelea).

Rais Samia amefanya uteuzi huo leo Jumamosi tarehe 15 Mei 2021, na kutangazwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu, Gerson Msigwa.

Sendiga anachukua nafasi ya Ali Hapi, aliyeteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora.

“Rais Samia amemteua Queen Cuthbert Sendiga, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa. Sendiga anachukua nafasi ya Ali Salum Hapi, ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa Tabora,” imesema taarifa ya Msigwa.

Sendiga alikuwa Mgombea Urais wa Tanzania, katika Uchaguzi Mkuu wa 2020, kupitia chama cha ADC.

Hatua hiyo ya Rais Samia kumteua Sendiga kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa, inatimiza ahadi yake aliyoitoa katika mkutano wake na Wazee wa Dar Es Salaam, kwamba katika Serikali yake atashirikisha wapinzani, ili kuleta Umoja wa Kitaifa.

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan

Rais Samia amefuata nyayo za mtangulizi wake, aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati John Magufuli, za kuteua viongozi wa Serikali kutoka vyama vya upinzani.

2017, Dk. Magufuli  alimteua aliyekuwa Mgombea Urais wa ACT-Wazalendo katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, Anna Mghwira kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilimanjaro.

Mghwira ameuongoza mkoa huo kuanzia mwaka 2017  hadi 2021, baada ya kustaafu.

Rais Samia amemteua aliyekuwa Katibu wa Bunge,  Stephen Kagaigai, kurithi mikoba ya Mghwira Kilimanjaro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!