Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Bosi zamani TRA ateuliwa Udart
Habari Mchanganyiko

Bosi zamani TRA ateuliwa Udart

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemteua Dk. Edwin Mhede kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (UDART). Anaripoti Hamis Mguta…(endelea).

Uteuzi wa Dk. Mhede, umetangazwa leo Jumamosi, tarehe 15 Mei 2021 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa ambaye amesema, anachukua nafasi ya John Nguya ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Kutenguliwa kwa uteuzi wa Nguya, umefanyika ikiwa ni takribani wiki mbili zimepita, tangu Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, kufanya ziara ya kutembelea mradi wa mabasi yaendayo haraka mkoani Dar es Salaam.

John Nguya

Katika ziara hiyo, Majaliwa alisema, Nguya ameshindwa kutimiza majukumu yake ipasavyo na kuufanya wakala huo, kutoa huduma chini na malengo na kuahidi kufikisha suala lake kwa mamlaka ya uteuzi kwa hatua zaidi.

Dk. Mhede, aliyekuwa Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ameteuliwa ikiwa zimepita siku 41 tangu alipomwondolewa TRA na nafasi yake kuteuliwa Alphayo Kidata.

Rais Samia, alimteua Kidata kuwa Kamishna wa TRA, tarehe 4 Aprili 2021.

Dk. Mhede, aliongoza TRA kuanzia 8 Januari 2019, akichukua nafasi ya Charles Kichere ambaye aliteuliwa kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Njombe. Kwa sasa Kichere ni Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Kabla ya uteuzi huo, Dk. Mhede alikuwa naibu katibu mkuu wizara ya viwanda na biashara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NMB yakabidhi vifaa vya ujenzi, samani kwa shule ya msingi Sinyaulime, Chuo cha FDC Morogoro

Spread the loveBENKI ya NMB imekabidhi vifaa vya ujenzi kwa shule ya...

Habari Mchanganyiko

NMB Bonge la Mpango – ‘Moto Uleule’ yazinduliwa, Milioni 180…

Spread the loveMSIMU wa tatu wa Kampeni ya kuhamasisha utamaduni wa Kuweka...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

error: Content is protected !!