Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko THRDC yalia udukuzi wa taarifa, TCRA yatoa neno
Habari Mchanganyiko

THRDC yalia udukuzi wa taarifa, TCRA yatoa neno

Onesmo Olengulumwa, Mratibu THRDC
Spread the love

 

MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umeiomba Serikali nchini humo, kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), iweke sheria zitakazodhibiti uingiliaji wa taarifa za watu kupitia mtandaoni. Anaripoti Regina Mkonde, Morogoro…(endelea).

Wito huo umetolewa na Mratibu wa THRDC, Onesmo Olengurumwa, katika mafunzo ya siku tatu ya wanahabari wa mtandaoni iliyofanyika mkoani Morogoro, kuanzia 10 Mei 2021 hadi leo Jumatano.

Olengurumwa ameishauri, TCRA ianzishe sheria ambayo italazimisha mtu kutopewa mawasiliano ya mtu kutoka katika kampuni za mawasiliano, hadi atakapopata kibali cha mahakama.

“TCRA mtusaidie kuimarisha ulinzi wa taarifa za mtandaoni, kuna sheria zipo ila inabidi ziwe tight (bana) yeyote anayetaka kuingilia tarifa za mtandaoni wapate kibali cha mahakama. Katika hili Tanzania tuko nyuma kwenye data protection laws (sheria za kulinda taarifa mtandaoni),” amesema Olengurumwa.

Mratibu huyo wa THRDC amesema, kwa sasa Tanzania inakabiliwa na changamoto ya taarifa na mawasiliano ya watu kuvujishwa huku akitolea mfano sakata la kuvuja kwa mazungumzo ya Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye na wenzake.

“Kampuni za simu zimepokea jumbe za watu wakitaka watoe mazungumzo ya watu, wanaambiwa watoe taarifa za wateja wao. Hii inakiuka haki za binadamu. Mtu akichunguza anatakiwa apate kibali cha mahakamani na kwa sababu maalum, labda za kiusalama wa nchi na kulinda haki za wengine,” amesema Onesmo na kuongeza:

“Mfano mazungumzo ya kina Nape ilitakiwa yabaki kwa wahusika tu kuliko kuyaleta kwa umma, hiyo ni kuingilia privace (faragha) ya mtu.”

Sakata la kuvuja kwa sauti yenye mazungumzo ya Nape na makatibu wakuu wastaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, Yusuf Makamba, wabunge wa CCM, Willium Ngeleja na aliyekuwa mwanachama wa chama hicho kabla ya kufukuzwa, Bernard Membe liliibuka Julai 2019, baada ya kusambazwa mitandaoni.

Mazungumzo hayo, yalihusu utendaji wa aliyekuwa mwenyekiti wa CCM na Rais wa Tanzania, Hayati John Pombe Magufuli, jinsi anavyoshindwa kukiongoza chama hicho na serikali.

Akijibu maombi hayo, Dk. Philip Filikunjombe, Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi na Utekelezaji wa Sheria wa TCRA amesema, atalifikisha suala hilo katika mamlaka hiyo kwa ajili ya kufanyiwa kazi.

“Kama taarifa za udukuzi unaendelea watu wanavujisha taarifa za watu, nitalifikisha ofisini kuona kama kuna watu wanafanya vitendo hivyo,” amesema Dk. Filikunjombe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!