Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Spread the love
RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amekwenda nchini Uganda, kuhudhuria sherehe ya kuapishwa kwa Rais mteule wa nchi hiyo, Yoweri Museveni. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Samia, ameondoka asubuhi ya leo Jumatano, tarehe 12 Mei 2021, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Sherehe za kuapishwa kwa Mseven, inafanyika leo Jumatano, Uwanja wa Kololo jijini Kampala.
Museveni anaapishwa kuendelea na uongozi wake aliouanza mwaka 1984, baada ya kushinda kiti cha Urais wa Uganda, kwenye Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 14 Januari 2021.
Yoweri Museveni
Katika uchaguzi huo, Museven alitangazwa mshindi baada ya kupata asilimia 58.6 ya kura huku aliyekuwa mpinzani wake wa karibu, Robert Kyagulanyi maarufu ‘Bob Wine’ akipata asilimia 34.8 ya kura.
More Stories
Msukuma: Mbowe alipa-miss Ikulu
Wabunge upinzani, CCM waungana kumpongeza Rais Samia
Dk. Mollel naye aagizwa kujibu maswali kwa ukamilifu