Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kenyatta amwambia Samia ‘safari hii tutafika mbali’
Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Kenyatta amwambia Samia ‘safari hii tutafika mbali’

Spread the love

 

RAIS wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema, ana matumaini kwa taifa lake na Tanzania kufika mbali kutokana na kuimarika ushirikiano. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Rais Kenyatta ametoa kauli hiyo leo tarehe 4 Mei 2021, baada ya kufanya mazungumzo na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan katika Ikulu ya Kenya. Rais Samia amefika nchini Kenya kwa zaira ya siku mbili (tarehe 4 – 5 Mei).

“…tunakuona kama dada yetu na nchi ya Tanzania na Kenya ni kitu kimoja, safari hiii tutaenda mbali sana kuhakiisha uhusiano wa nchi hizi unaendelea kuimarisha,” amesema Rais Kenyatta.

Akieleza mambo kadhaa aliyozungumza na Rais Samia, Rais Kenyatta amesema, wamekubaliana mambo mengi kwa lengo la kutimiza malengo ya waasisi wa mataifa haya mawili (Kenya na Tanzania).

“Tumezungumza kutahakikisha mambo ya biashara, uchumi, ya kitamaduni ambayo yamesaidia kujenga taifa letu la Kenya na Tanzania yanakuwa kwa manufaa yetu sisi wote.

“Tumekubaliana pia kuhusu masuala ya mawasiliano, namna ya kuimarisha safari za ndege, safari za reli, safari za baharini na safari za barabara,” amesema Rais Kenyatta.

Amesema, katika mazungumzo yao wamekubaliana kufanya haraka ya kuanzisha ujenzi wa barabara kutoka Malindi kuelekea Lungalunga mpaka kufika Bagamoyo.

“Tukasema, tutafurahia sana tukiona kuanzishwa safari zetu zile zilizokuwa kule Ziwa Victoria wakati wananchi na mzigo ilikuwa ikitembea kutoka upande wa Jinja kuja Kisumu kuelekea kule Mwanza na Bukoba,” amesema.

Kiongozi huyo wa Kenya amesema, amezungumza na Rais Samia kuhusu masuala ya usalama kwa nchi zote mbili ikiwa ni pamoja na kukabiliana na vitendo vya kigaidi.

“Tumeweka mikataba kuhusu kujenga bomba la gesi kutoka Dar es Salaam mpaka Mombasa, na hiyo itarahisisha bei na kusaidia pia viwanda vyetu kupata nishati,” amesema na kwamba, suala la utalii ni miongoni mwa mambo waliyokubaliana na kiongozi wa Tanzania (Rais Samia).

Rais Kenyatta ameonesha furaha kukutana na Rais Samia kwa kuwa, ni safari ya kwanza kutembelewa na rais mama wa kwanza Afrika Mashariki kuwa rais.

“Tunakupongeza sana kwa nafasi uliyopatiwa kuongoza Tanzania pia tunakupongeza kwa uchaguzi wako hivi karibuni kuwa mwenyekiti wa chama tawala – CCM, tunakuhakikishia Kenya na serikali yangu itakuwa mstari wa mbele kushirikiana,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!