Wednesday , 1 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wafanyakazi Dodoma yaomba nyongeza ya mishahara
Habari Mchanganyiko

Wafanyakazi Dodoma yaomba nyongeza ya mishahara

Spread the love

 

VYAMA vya wafanyakazi Mkoa wa Dodoma, wameiomba Serikali kuona uwezekano wa kuongeza mishahara kama inavyotakiwa kisheria. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Wametoa ombi hilo, leo Jumamosi, tarehe 1 Mei 2021, wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Mei Mosi yaliyofanyika kimkoa katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya Mei Mosi 2021 ni; Maslahi bora, mishahara juu, kazi iendelee.

Lizz Msechu, mwenyekiti Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), Mkoa wa Dodoma amesema, kitendo cha wafanyakazi kutopandishiwa mishahara yao kwa kipindi cha miaka zaidi ya mitano, kinawafanya wafanyakazi kuishi maisha mabaya.

“Tunaomba serikali ione umuhimu wa kurejesha utaratibu wa kuongeza nyongeza za mishahara ili kuwe za kuwafanya wafanyakazi kuweza kuishi maisha ambayo yatakuwa na unafuu”amesema Msechu.

Pia, amesema wafanyakazi wanaiomba serikali kuona namna ya kubadili ulipaji wa kodi kwani watumishi wanajikuta wakilipa kodi mara mbili kwa maana ya kulipa kodi moja kwa moja inayokatwa kwenye mshahara na kulipa kodi wanapokwenda kununua bidhaa.

Katika hatua nyingine, amesema baadhi ya waajiri wamekuwa hawataki kuanzishwa kwa mabaraza ya kazi jambo ambalo linakinzana na utaratibu.

Akizungumzia kuhusu mafao ya wastaafu, Msechu amesema ni changamoto kubwa kwa kuwacheleweshea mafao yao wastaafu mafao tao.

Dk. Binirithi Mahenge, mkuu wa Mkoa wa Dodoma akijibu maombi hayo ya wafanyakazi amewaagiza waajiri wote kuhakikisha wanaanzisha mabaraza ya wafanyakazi katika sehemu za kazi.

Mbali na hilo, ameziagiza taasisi zote zinazotoa mafao ya wastaafu kuhamikisha wanatoa mafao kwa wakati badala ya kuwacheleweshea mafao yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!