Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Shibuda: Kuna ombwe la siasa za utaifa, uzalendo
Habari za Siasa

Shibuda: Kuna ombwe la siasa za utaifa, uzalendo

Spread the love

 

MWENYEKITI wa Baraza la Vyama vya Siasa nchini Tanzania, John Shibuda, amesema, kuna ombwe la makada wa kuendeleza siasa za utaifa na uzalendo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Shibuda ametoa kauli hiyo leo Jumatatu tarehe 26 Aprili 2021, wakati akichangia katika Kongamano la Maahimisho ya Miaka 57 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, jijini Dodoma.

Mwanasiasa huyo mkongwe nchini Tanzania, amesema ombwe hilo limesababishwa na marais waliopita, Rais wa Awamu ya Pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi, Hayati Benjamin Mkapa (Awamu ya Tatu), Dk. Jakaya Kikwete (Awamu ya Nne) na Hayati Dk. John Magufuli (Awamu ya Tano), kutoandaa makada hao.

“Mimi ni Mwenyekiti wa Baraza la Vyama ya Siasa Tanzania, nasikitika kusema Tanzania ina ombwela sintofahamu la miaka 35.”

“Mzee Mwinyi hakuandaa makada wa kuendeleza maana ya siasa za utaifa na uzalendo. Mzee Mkapa hakufanya hivyo, Dk. Kikwete hakutekeleza hilo, hayati Magufuli hakufanya hilo. Sijui Awamu ya Sita,” amesema Shibuda.

Awamu ya sita, inaongea na Rais Samia Suluhu Hassan.

 

Kuhusu maadhimisho ya muungano huo, Shibuda ameishauri Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira, ijipange katika kuhakikisha vitabu vilivyoandikwa historia ya muungano inawafikia Watanzania wote, hasa waliozaliwa baada ya muungano huo.

“Mfano leo tuna wanafunzi wasiopungua 200 hapa (kwenye kongamano), ukiwauliza nini maana ya tunu ya muungano na kwa nini muungano ni tunu ya taifa, utapata majibu 200 tofauti, lakini ukimkuta shia au suni ukimuuliza kuhusu mtume Mohamed (S.A.W), makutano yao yako kwenye Msahafu.

“Wakristo makutano ya madhehebu yote yako katika kitabu kitakatifu cha Bibilia, Watanzania wa mfumo wa vyama vingi wa makundi ya wanaharakati mbalimbali hivi makutano yetu ni kwenye kitu gani?” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!