Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Shibuda: Kuna ombwe la siasa za utaifa, uzalendo
Habari za Siasa

Shibuda: Kuna ombwe la siasa za utaifa, uzalendo

Spread the love

 

MWENYEKITI wa Baraza la Vyama vya Siasa nchini Tanzania, John Shibuda, amesema, kuna ombwe la makada wa kuendeleza siasa za utaifa na uzalendo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Shibuda ametoa kauli hiyo leo Jumatatu tarehe 26 Aprili 2021, wakati akichangia katika Kongamano la Maahimisho ya Miaka 57 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, jijini Dodoma.

Mwanasiasa huyo mkongwe nchini Tanzania, amesema ombwe hilo limesababishwa na marais waliopita, Rais wa Awamu ya Pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi, Hayati Benjamin Mkapa (Awamu ya Tatu), Dk. Jakaya Kikwete (Awamu ya Nne) na Hayati Dk. John Magufuli (Awamu ya Tano), kutoandaa makada hao.

“Mimi ni Mwenyekiti wa Baraza la Vyama ya Siasa Tanzania, nasikitika kusema Tanzania ina ombwela sintofahamu la miaka 35.”

“Mzee Mwinyi hakuandaa makada wa kuendeleza maana ya siasa za utaifa na uzalendo. Mzee Mkapa hakufanya hivyo, Dk. Kikwete hakutekeleza hilo, hayati Magufuli hakufanya hilo. Sijui Awamu ya Sita,” amesema Shibuda.

Awamu ya sita, inaongea na Rais Samia Suluhu Hassan.

 

Kuhusu maadhimisho ya muungano huo, Shibuda ameishauri Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira, ijipange katika kuhakikisha vitabu vilivyoandikwa historia ya muungano inawafikia Watanzania wote, hasa waliozaliwa baada ya muungano huo.

“Mfano leo tuna wanafunzi wasiopungua 200 hapa (kwenye kongamano), ukiwauliza nini maana ya tunu ya muungano na kwa nini muungano ni tunu ya taifa, utapata majibu 200 tofauti, lakini ukimkuta shia au suni ukimuuliza kuhusu mtume Mohamed (S.A.W), makutano yao yako kwenye Msahafu.

“Wakristo makutano ya madhehebu yote yako katika kitabu kitakatifu cha Bibilia, Watanzania wa mfumo wa vyama vingi wa makundi ya wanaharakati mbalimbali hivi makutano yetu ni kwenye kitu gani?” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!