Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko 49 wakamatwa Dar tuhuma wizi, ununuzi vifaa vya magari
Habari Mchanganyiko

49 wakamatwa Dar tuhuma wizi, ununuzi vifaa vya magari

Spread the love

 

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge amesema, zaidi ya watu 49, wanashikiliwa na Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa tuhuma za wizi na ununuzi wa vifaa vya magari na pikipiki. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).

Ni baada ya operesheni iliyofanywa na polisi chini ya kamanda wa polisi wa kanda hiyo, Lazaro Mambosasa, kukamata vifaa mbalimbali vya magari pamoja na pikipili zilizoibiwa.

Akitoa Mrejesho wa Operesheni, RC Kunenge amesema, kupitia msako uliofanyika wamefanikiwa kukamata vifaa mbalimbali ikiwemo taa za magari, Side mirror, power windows, Bampa, Vioo, Gearbox, Radio, Rim na vifaa vingine vingi.

Kutokana na hilo, Kunene amesema, kamwe hatoruhusu uhuni na wizi wa namna hiyo kuendelea mkoani mwake ambapo pia ametoa wito kwa wakuu wa mikoa wenzake kutokubali vifaa vya wizi kuuzwa katika mikoa yao.

Kwa upande wake, Kamanda Mambosasa amesema, miongoni mwa waliokamatwa ni wauzaji wa vifaa vya wizi ambao wamekuwa wakiwatuma wezi kwenda kuiba magari na vifaa.

Katika msako huo pia, wamefanikiwa kukamata gari iliyokuwa ikitumika kusafirisha vifaa vya wizi pamoja na Pikipiki zilizoibiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!