Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko 49 wakamatwa Dar tuhuma wizi, ununuzi vifaa vya magari
Habari Mchanganyiko

49 wakamatwa Dar tuhuma wizi, ununuzi vifaa vya magari

Spread the love

 

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge amesema, zaidi ya watu 49, wanashikiliwa na Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa tuhuma za wizi na ununuzi wa vifaa vya magari na pikipiki. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).

Ni baada ya operesheni iliyofanywa na polisi chini ya kamanda wa polisi wa kanda hiyo, Lazaro Mambosasa, kukamata vifaa mbalimbali vya magari pamoja na pikipili zilizoibiwa.

Akitoa Mrejesho wa Operesheni, RC Kunenge amesema, kupitia msako uliofanyika wamefanikiwa kukamata vifaa mbalimbali ikiwemo taa za magari, Side mirror, power windows, Bampa, Vioo, Gearbox, Radio, Rim na vifaa vingine vingi.

Kutokana na hilo, Kunene amesema, kamwe hatoruhusu uhuni na wizi wa namna hiyo kuendelea mkoani mwake ambapo pia ametoa wito kwa wakuu wa mikoa wenzake kutokubali vifaa vya wizi kuuzwa katika mikoa yao.

Kwa upande wake, Kamanda Mambosasa amesema, miongoni mwa waliokamatwa ni wauzaji wa vifaa vya wizi ambao wamekuwa wakiwatuma wezi kwenda kuiba magari na vifaa.

Katika msako huo pia, wamefanikiwa kukamata gari iliyokuwa ikitumika kusafirisha vifaa vya wizi pamoja na Pikipiki zilizoibiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!