Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko 49 wakamatwa Dar tuhuma wizi, ununuzi vifaa vya magari
Habari Mchanganyiko

49 wakamatwa Dar tuhuma wizi, ununuzi vifaa vya magari

Spread the love

 

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge amesema, zaidi ya watu 49, wanashikiliwa na Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa tuhuma za wizi na ununuzi wa vifaa vya magari na pikipiki. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).

Ni baada ya operesheni iliyofanywa na polisi chini ya kamanda wa polisi wa kanda hiyo, Lazaro Mambosasa, kukamata vifaa mbalimbali vya magari pamoja na pikipili zilizoibiwa.

Akitoa Mrejesho wa Operesheni, RC Kunenge amesema, kupitia msako uliofanyika wamefanikiwa kukamata vifaa mbalimbali ikiwemo taa za magari, Side mirror, power windows, Bampa, Vioo, Gearbox, Radio, Rim na vifaa vingine vingi.

Kutokana na hilo, Kunene amesema, kamwe hatoruhusu uhuni na wizi wa namna hiyo kuendelea mkoani mwake ambapo pia ametoa wito kwa wakuu wa mikoa wenzake kutokubali vifaa vya wizi kuuzwa katika mikoa yao.

Kwa upande wake, Kamanda Mambosasa amesema, miongoni mwa waliokamatwa ni wauzaji wa vifaa vya wizi ambao wamekuwa wakiwatuma wezi kwenda kuiba magari na vifaa.

Katika msako huo pia, wamefanikiwa kukamata gari iliyokuwa ikitumika kusafirisha vifaa vya wizi pamoja na Pikipiki zilizoibiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NMB Bonge la Mpango – ‘Moto Uleule’ yazinduliwa, Milioni 180…

Spread the loveMSIMU wa tatu wa Kampeni ya kuhamasisha utamaduni wa Kuweka...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

error: Content is protected !!