Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia aendelea kuteua viongozi
Habari za Siasa

Rais Samia aendelea kuteua viongozi

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Uteuzi huo, umetangazwa jana Alhamisi, tarehe 22 Aprili 2021 na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Walioteuliwa ni;

1. Amemteua Prof. Henry Fatael Mahoo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Uongozi ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji.

2. Amemteua Jaji wa Mahakama ya Rufani, Dk. Gerald Ndika kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto.

Dk. Ndika ameteuliwa kushika wadhifa huo kwa kipindi cha pili baada ya kipindi cha kwanza kumalizika.

3. Amemteua Prof. Aurelia K. Kamuzora kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kahawa Tanzania.

4. Amemteua Prof. Idris S. Kikula kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Madini Tanzania.

Prof. Kikula ameteuliwa kushika wadhifa huo kwa kipindi cha pili baada ya kipindi cha kwanza kumalizika.

Msigwa amesema, Rais Samia amewateua Prof. Abdulkarim Mruma na Janeth Lekashingo kuwa wajumbe wa Tume ya Madini Tanzania.

Uteuzi wa viongozi hawa umeanza tarehe 20 Aprili, 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

error: Content is protected !!