Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia aonya wanaotumia mitandao ya kijamii kuchonganisha
Habari za Siasa

Rais Samia aonya wanaotumia mitandao ya kijamii kuchonganisha

Samia Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan, ameonya Watanzania wanaotumia mitandao ya kijamii kuchonganisha watu. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Kiongozi huyo wa Tanzania ametoa onyo hilo leo Alhamisi tarehe 22 Aprili 2021, akihutubia Bunge jijini Dodoma.

Rais Samia amesema hayo wakati akikemea taarifa za uzushi juu ya chanzo cha kifo cha aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati Dk. John Magufuli, kilichotokea tarehe 17 Machi 2021, kwenye Hospitali ya Mzena mkoani Dar es Salaam.

“Nikemee vikali wale walioko kwenye mitandao, ndugu zangu dini zetu zinasema na ni kanuni ya maisha, tunakuja duniani na tunaondoka duniani.

nimekuwa nikiona kwenye mitandao na nadhani wanaofanya hivyo wanajua kwamba hatutaweza kuwapata, wanatumia mifumo huko mingine ambayo bado hatujawa na uwezo wa kuwatafuta lakini niwamabie tutawatafuta,” amesema Rais Samia.

Mrithi huyo wa Dk. Magufuli amewataka watu hao kama wanaushahidi wa kutosha wauwasilishe katika vyombo vya uchunguzi kwa ajili ya kufanyiwa kazi.

“Nimekuwa nikiona kwenye mitandao taarifa za uchonganishi, taarifa tuliyopewa na madaktari wetu ya kifo cha Dk. Magufuli ni kutokana na tatizo la udhaifu wa moyo ambalo ameishi nalo  kwa muda wa miaka 10.

Kuna watu wamejitokeza kwenye mitandao huko fulani na fulani wamempa sumu, fulani na fulani walikuwa wametega kitu hiki. Sasa niwaambie kama wanataraifa za maana waje tuwasikilize, vyombo vya upelelezi na uchunguzi vipo waje tuwasilikize,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!