Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia aendelea kuteua viongozi
Habari za Siasa

Rais Samia aendelea kuteua viongozi

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Uteuzi huo, umetangazwa jana Alhamisi, tarehe 22 Aprili 2021 na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Walioteuliwa ni;

1. Amemteua Prof. Henry Fatael Mahoo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Uongozi ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji.

2. Amemteua Jaji wa Mahakama ya Rufani, Dk. Gerald Ndika kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto.

Dk. Ndika ameteuliwa kushika wadhifa huo kwa kipindi cha pili baada ya kipindi cha kwanza kumalizika.

3. Amemteua Prof. Aurelia K. Kamuzora kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kahawa Tanzania.

4. Amemteua Prof. Idris S. Kikula kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Madini Tanzania.

Prof. Kikula ameteuliwa kushika wadhifa huo kwa kipindi cha pili baada ya kipindi cha kwanza kumalizika.

Msigwa amesema, Rais Samia amewateua Prof. Abdulkarim Mruma na Janeth Lekashingo kuwa wajumbe wa Tume ya Madini Tanzania.

Uteuzi wa viongozi hawa umeanza tarehe 20 Aprili, 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!