Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia afungulia vyombo vya habari
Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia afungulia vyombo vya habari

Samia Suluhu Hassani, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameiagiza Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuvifungulia vyombo vyote vya habari vilivyofungiwa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Samia ametoa agizo hilo leo Jumanne, tarehe 6 Aprili 2021, Ikulu ya Dar es Salaam, mara baada ya kumaliza kuwaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni.

Akigusia sekta ya habari, Rais Samia amesema “wizara ya habari, mnapaswa kusimamia vyombo vya habari, nasikia kuna vyombo vya habari huko mmevifungia, vifungulieni lakini vifuate sheria na kanuni.”

Rais Samia amesema, “tusiwape mdomo mdomo wa kusema tunabinya uhuru wa habari na nataka kanuni ziwe wazi, ili mtu akifungiwa ajue kosa na adhabu yake. Tusifungie tu kibabe.”

Baadhi ya magazeti yaliyofungiwa ni; MwanaHALISI, Mawio, Tanzania Daima na Mseto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

error: Content is protected !!