Tuesday , 16 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia atoa msimamo kuhusu corona
Habari za Siasa

Samia atoa msimamo kuhusu corona

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema, ataunda kamati maalum ya kufanyia utafiti ugonjwa wa maambukizi ya virusi vya corona (COVID-19) kwani “Tanzania siyo kisiwa.” Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Samia ametoa msimamo huo leo Jumanne, tarehe 6 Aprili 2021, katika hotuba yake baada ya kumaliza kuwaapisha viongozi mbalimbali aliowateua hivi karibuni wakiwemo Makati wakuu, naibu wao na wakuu wa taasisi kadhaa.

Akigusia suala la corona, Rais Magufuli amesema “nakusudia kuunda kamati ya wataalamu, waliangalie suala la COVID kitaalamu zaidi na kwa ukubwa wake halafu watushauri. Hatufai kulikataa au kulikubali pasina kulifanyia utafiti.”

“Hatuwezi kujitenga kama kisiwa na hatuwezi kupokea kila tunachoambiwa bila kufanya ya kwetu. Rais Kikwete alituambia ya kuambiwa…,” amehoji Rais Samia huku akijibiwa “changanya na yako.”

Msimamo alioutoa Rais Samia, ni tofauti na ule wa serikali iliyopita ambayo ilishindwa kuweka msimamo wake kuhusu corona na ilizuia utoaji wa taarifa na takwimu zozote kuhusu ugonjwa huo.

Pia, haikutumia njia za kisayansi kukabiliana na ugonjwa huo hatari na badala yake, ilihimiza matumizi ya njia za tiba za asili hasa za kujifukiza “kupiga nyungu” na maombi yaliyofanywa na viongozi wa dini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia amfariji mjane wa Musa Abdulrahman

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumanne amempa pole Mwanakheri Mussa...

Habari za Siasa

Nape: Wanasiasa, wanahabari, wafanyabiashara mteteeni Samia

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano,...

Habari za Siasa

CAG: TAWA imegawa vibali vya uwindaji bila idhini ya waziri

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

Habari za Siasa

TAMISEMI yatenga bil. 17.79 kwa ajili uchaguzi serikali za mitaa

Spread the loveWIZARA Ofisi ya Rais-TAMISEMI, imetenga fedha kiasi cha Sh. 17.79...

error: Content is protected !!