Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri Mpango mgonjwa, Magufuli asoma ‘sms’ aliyotumiwa
Habari za Siasa

Waziri Mpango mgonjwa, Magufuli asoma ‘sms’ aliyotumiwa

Spread the love

 

JOHN Magufuli, Rais wa Tanzania, amelazimika kusoma hadharani ujumbe aliotumiwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Phillip Mpango, ili kukanusha taarifa za uongo zilizodai waziri huyo amefariki dunia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Magufuli amesoma ujumbe huo leo Ijumaa tarehe 19 Februari 2021, kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam, katika Ibada ya kuuaga mwili wa aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi, aliyefariki dunia tarehe 17 Februari mwaka huu, Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma.

Hivi karibuni katika mitandao ya kijamii, zilisambaa taarifa za uongo zilizodai Dk. Mpango amefariki dunia.

Kufuatia uvumi huo, Mkuu huyo wa nchi amesema, Dk. Mpango ni kweli amelazwa hospitalini jijini Dodoma na leo asubuhi, alimtumia ujumbe mfupi wa maandishi, akimjulisha kwamba anaendelea vizuri na matibabu.

“Tumefikia mahali tunatishana sana, leo nilitumwia meseji na Waziri wa Fedha, Dk. Mpango ambaye amelazwa Dodoma, na ninaomba niisome hapa kwa faida ya wale waliokwua wana-Twitte kwamba amekufa,” amesema Rais Magufuli.

Baada ya kauli hiyo, alitoa simu yake mfukoni na kuanza kuusoma “Leo asubuhi ananiambia mheshimiwa rais, ahsante sana, nimepata ujumbe wako kupitia mke wangu, kwa neema ya Mungu naendelea vizuri. Ninakula, nafanya mazoezi ya kifua na kutembea.”

Kuhusu watu waliomzushia kifo Dk. Mpango, Rais Magufuli amesema waziri huyo amewaombea msamaha kwa Mungu.

Rais Magufuli amenukuu ujumbe huo wa Dk. Mpango uliosema “hao wanaonizushia kifo kwenye mitandao, niliwaombea msamaha kwa Yesu wakati wa sala ya jioni jana.”

“Huyo ambaye aliambiwa jana amekufa, yeye amesema katika sala yake jana jioni aliwaombea msamaha kwa Yesu,” amesema Rais Magufuli

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!