Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dada wa Spika Ndugai afariki, azikwa
Habari za Siasa

Dada wa Spika Ndugai afariki, azikwa

Spread the love

 

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa ameshiriki mazishi ya Mary Ndugai, dada wa Spika wa Bunge, Job Ndugai. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mpwapwa … (endelea).

Mary alifariki dunia Jumamosi iliyopita ya tarehe 23 Januari 2021, wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma.

Mazishi hayo ya Mary yamefanyika leo Jumatatu, 25 Januari 2021, katika makaburi ya Ving’awe wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na Bunge.

Akizungumza baada ibada ya kumuombea marehemu Mary iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) jimbo la Mpwapwa, Waziri Mkuu, Majaliwa amewaomba wafiwa wawe na subira na utulivu katika kipindi hiki kigumu.

“Nimekuja kuungana nanyi kwa niaba ya Mheshimiwa Rais John Magufuli na Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan kutoa pole kwa Mheshimiwa Spika Job Ndugai kufuatia msiba mzito wa kuondokewa na dada yake mpendwa Mary.”

Waziri Mkuu amesema, msiba huo ni mzito na jukumu kubwa ni kumuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu pahala pema, hivyo amewaomba watoto wa marehemu, ndugu na jamaa wawe watulivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.

Kwa upande wake, Spika wa Bunge, Job Ndugai amewashukuru viongozi wa dini, Serikali na waombolezaji kwa kujitokeza na kuifariji familia kufuatia msiba huo.

Pia, amewashukuru madaktari na wauguzi wa Hospitali ya wilaya ya Mpwapwa ambapo marehemu alikuwa akitibiwa.

Viongozi wengine waliohudhuria mazishi hayo ni Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, Waziri wa Mambo ya Ndani, George Simbachawene, Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Mwigulu Nchemba, Katibu wa Bunge, Stephen Kigaigai na baadhi ya wabunge.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!